IQNA

13:00 - April 29, 2009
Habari ID: 1771301

Nigeria ina wahifadhi wengi zaidi wa Qur'ani duniani

Mkuu wa Jumuiya ya Wanazuoni wa Kiislamu ya jimbo la Kano nchini Nigeria amesema kuwa kwa mujibu wa takwimu zilizopo, nchi hiyo ndiyo iliyo na idadi kubwa zaidi ya wahifadhi Qur'ani duniani na kwamba wengi wao wako katika jimbo hilo la Kano.

Kwa mujibu wa tovuti ya Allafrika, Sheikh Ibrahim Khalil ameyasema hayo alipokutana na mkuu wa Jumuiya ya Wahifadhi wa Qur'ani ya Nigeria na kuongeza kuwa hiyo ni neema kubwa iliyopewa nchi hiyo ya Kiafrika na Mwenyezi Mungu, neema ambayo kwa bahati mbaya amesema haitumiwi vyema wala kuungwa mkono ipaswavyo na viongozi husika.
Sheikh Ibrahim Khalil amewataka Waislamu wote wa Nigeria kuunga mkono na kuwasaidia wahifadhi Qur'ani na kutowazingatia tu katika mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Pia ametoa habari nzuri ya wahifadhi wa Qur'ani kupewa vyeti vya kiwango cha udakta na serikali ya nchi hiyo. 396145
captcha