IQNA

13:52 - May 12, 2009
Habari ID: 1777420

Kiongozi wa Mabudha Duniani akosoa utumiwaji mbaya wa jihadi ya Kiislamu

Gazet la Marekani la Boston Globe, limemnukuu Dalai Lama, Kiongozi wa Mabudha Duniani ambaye pia ni mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel akisema kuwa fikra ya jihadi katika Uislamu inatumiwa vibaya sana ulimwenguni.

Akizungumza hivi karibuni mbele ya wanachuo wa Chuo Kikuu cha Havard nchini Marekani, Dalai Lama amekosoa vikali utumiaji mbaya wa jihadi ya Kiislamu na kuongeza kuwa kila mtu anayeelewa vyema sheria za Kiislamu anafahamu kwamba jihadi ina maana ya kujitetea. Amesema katika miaka ya hivi karibuni jihadi imekuwa ikitumiwa vibaya zaidi ulimwenguni kuliko jambo jingine lolote. Dalai Lama pia amesisitiza kwamba neno 'Allah' na kumsifu Mwenyezi Mungu lina maana ya mahaba na mapenzi makubwa yasiyo na mwisho na kwamba Uislamu unawafundisha wafuasi wake kuwapenda wanadamu wote wawe, ni Waislamu au la.
Katika maandishi yake pia, Karen Armstrong, mwandishi mashuhuru wa Uingereza kuhusiana na masuala ya dini za mbinguni, amekosoa vikali upotoshaji na matumizi mabaya ya neno jihadi katika nchi za Magharibi na kusisitiza kwamba upotoshaji huo unafanywa makusudi kwa madhumuni ya kufikia malengo maalumu. 403367
captcha