Kwa mujibu wa gazeti la as-Sharqul Ausat, mazungumzo kati ya Magharibi na ulimwengu wa Kiislamu yanapaswa kufanyika kwa msingi wa kuimarisha uhusiano mwema na kwa madhumuni ya kuheshimiana na kufahamiana pande mbili. Al-Jundi amezitaka nchi za Kiislamu kuimarisha mawasiliano na ushirikiano wao na jamii pamoja na jumuiya za Kiislamu zinazoishi katika nchi za Ulaya na Marekani ili kukabiliana na mielekeo iliyo dhidi ya Uislamu katika nchi za Magharibi. Al-Jundi amesisitiza mwishoni juu ya udharura wa kuanzishwa televisheni ya satalaiti kwa madhumuni ya kutangaza matangazo na vipindi vya Kiislamu ili kuwafahamisha raia wa nchi za Magharibi mafundisho halisi ya Kiislamu. 407641