Geert Wilders, mbunge mwenye misiamamo ya kupindukia mipaka dhidi ya Uislamu wa Uholanzi na mtengenezaji wa filamu ya matusi na dharau dhidi ya Qur'ani Tukufu ametangaza kuwa atashiriki katika maandamano yajayo yaliyo dhidi ya Uislamu yaliyopangwa kufanyika nchini Marekani tarehe 11 Septemba mwaka huu ili kuonyesha mfungamano wake na wapinzani wa Uislamu nchini humo.
Wilders pia amepangiwa kuzungumza katika maandamano hayo yaliyopamgwa kufamyika mjini New York. Maandamano hayo yameandaliwa na maadui pamoja na wapinzani wa Uislamu wanaopinga kujengwa kwa msikiti na kituo cha Kiislamu cha gorofa 13 mjini New York. Wanadai kwamba wanataka kupambana na kile wametaja kuwa kufanywa Marekani kuwa nchi ya Kiislamu. Inasemekana kwamba meya na taasisi kadhaa za serikali katika mji wa New York zimekubaliana na suala la ujenzi wa msikiti na kituo hicho cha Kiislamu katika eneo na Manhattan katika mji huo, lakini makundi hayo yenye misimamo mikali na ya kiuadui dhidi ya Uislamu yanapinga vikali jambo hilo.628113