IQNA

17:45 - August 09, 2010
Habari ID: 1970080

Kongamano la "Nafasi ya Kisiasa ya Wanawake Waislamu" kufanyika Uingereza

Kongamano la Kimataifa la "Nafasi ya Kisiasa ya Wanawake Waislamu" litafanyika Uingereza kwa himaya ya Kituo cha Utafiti kuhusu Uhusiano wa Kikaumu katika Chuo Kikuu cha Warwick katika mji wa Birmingham .

Kongamano hilo linatazamiwa kufanyika tarehe 20/21 Septemba na litahudhuriwa na wasomi kutoka maeneo mbali mbali ya dunia. Washiriki watachunguza nafasi ya kisiasa ya wanawake Waislamu katika jamii za Uingereza, Ufaransa na nchi nyingine kubwa duniani.
Masuala yatakayojadiliwa katika kongamano hilo ni pamoja na kushiriki wanawake Waislamu katika shughuli za kijamii na kisiasa katika nchi zisizo za Kiislamu hasa Uingereza na Ufaransa, njia za kuimarisha ushirikiano baina ya wanaharakati wanawake Waislamu na mashirika ya kutetea haki za wanawake.
629394







captcha