Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA kuna mpango wa masomo ya miaka miwili, mitatu na minne kwa wanaotaka kuhifadhi Qur'ani Tukufu. Kwa mujibu wa mpango huo Maustadhi wa Taasisi ya Darul Qur'an ya Iran watakuwa wakipiga simu kwenye nyumba za washiriki na kwa njia hiyo kutoa mafunzo ya kuhifadi Qur'ani Tukufu.
Washiriki watahifadhi Qur'an kwa mujibu wa sura na watasahihishwa makosa yao na kusaidiwa kuhifadhi Qur'ani kwa njia rahisi. 638413