Mkataba huo ulitiwa saini katika kikao cha tano cha Mawaziri wa Elimu ya Juu wa nchi wanachama wa Umoja wa Nchi za Kiislamu OIC huko Kuala Lumpur Malaysia. Kwa mujibu wa mkataba huo, mashirika mawili hayo ya OIC katika kipindi cha mwaka 2010 hadi 2011 yatashirikiana kwa karibu katika nyanja za elimu na utamaduni ikiwemo tiba, sayansi ya anga, teknolojia ya kisasa, usimamizi wa maji na elimu ya mawasiliano na kilimo katika nchi za Kiislamu. 679242