IQNA

Idadi ya wanaotaka Qur'ani duniani yaongezeka

11:32 - November 11, 2010
Habari ID: 2029826
Mashirika ya kuzalisha makaratasi duniani na taasisi za uchapisaji za kimataifa zimetangaza kuwa zimeanzisha vitengo maalumu vya kuchapisha Qur'ani Tukufu kufutia ongezeko kubwa la watu wanaotaka kusoma kitabu hicho kitakatifu.
Gerhard Wolf Mkurugenzi wa Utafutaji Masoko katika shirika kubwa la Ulaya la kuzalisha kakaratasi la Delfortgoup mjini Austria ameliambia Shirika la Habari za Qur'ani la Kimataifa IQNA, kwamba, 'tunafuatilia kwa karibu suala la kuongezeka maombi ya uchapishaji Qur'ani Tukufu'.
Akizungumza pambizoni mwa mashindano na maonyesho ya uchapishaji misahafu yaliyofanyika mjini Tehran Wolf ameongeza kuwa, 'kiwango cha maombi ya kuchapishwa Qur'ani Tukufu kimeongezeka zaidi ya Bibilia'. Amesema kwa kuzingatia kuwa idadi ya Waislamu duniani imepindukia Bilioni 1.7 na inazidi kuongezeka, kuna haja ya kuongeza vituo vya kuchapisha misahafu.
Mashindano na maonyesho ya uchapishaji misahafu yalimalizika siku ya Jumatano mjini Tehran.
693256
captcha