IQNA

12:42 - November 15, 2010
Habari ID: 2032043

Katibu Mkuu wa ISESCO asisitiza juu ya umoja wa umma wa Kiislamu

Katibu Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Kiislamu la Elimu, Utamaduni na Sayansi ISESCO Bw. Abdul Aziz Othman al Tuwaijri ametoa salamu za heri na fanaka kwa mnasaba wa Idul Adh'ha na kusema kuna ulazima wa kuwepo umoja zaidi katika umma wa Kiislamu.

Kwa mujibuwa wa tovuti ya ISESCO, al Tuwaijri katika ujumbe wake amesema umma wa Kiislamu unahitajia umoja na mshikamano zaidi kupitia kujiepusha na mifarakano. Amesema umoja utauwezesha umma wa Kiislamu kufikia malengo yake.
Katibu Mkuu wa ISESCO pia ameashiria nutka zinazowakutanisha pamoja za Waislamu wote katika fremu ya johari ya dini tukufu ya Kiislamu, Qur'ani na Qibla na kusisitiza kuwa, 'mifarakano inaenda kinyume na mafundisho ya Qur'ani na kudhoofisha umma wa Kiislamu.
Kuhusu kadhia ya Palestina, mkuu huyo wa ISESCO amesema kuna haja ya kuwepo umoja miongoni mwa makundi ya Wapalestina ili waweza kukabiliana na uhasama wa utawala wa Kizayuni. Aidha ametoa wito kwa nchi za Kiislamu kuwasaidia watu wa Palestina katika kukabiliana na Wazayuni. al Tuwaijri amesema, 'kukombolewa Quds Tukufu na ardhi zote za Palestina ni wadhifa mtakatifu na asili wa umma wa Kiislamu.
695582
captcha