IQNA

11:33 - November 16, 2010
Habari ID: 2032817

Katibu Mkuu wa MWL atoa wito wa umoja wa Waislamu duniani

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Waislamu Duniani (MWL) Dkt. Abdullah bin Abdulmuhsin al-Turki ametoa wito kwa viongozi na wananchi wa nchi za Kiislamu kunufaika na msimu wa hija kwa kujadili masuala ya umma, kuunganisha Waislamu, kuunga mkono harakati za Kiislamu na kushirikiana katika kukabiliana na changamoto.

Mwito huo wa al Turki uko katika barua aliyowaandikia viongozi wa nchi za Kiislamu kwa mnasaba wa siku ya Arafat.
Wakati huo huo Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiislamu (OIC) Prof. Ekmeleddin Ihsanoglu na Katibu Mkuu wa Shirika la Nchi za Kiislamu la Elimu, Sayansi na Utamaduni (ISESCO) Dkt. Abdul Aziz Othman al Tuwaijri wametoa salamu za heri na fanaka kwa Waislamu wote kwa mnasaba wa Idul Adh'ha na kutoa wito wa umoja na mshikamano katika umma wa Kiislamu.

696394
captcha