IQNA

"Mtume Muhammad SAW katika Ukristo" chachapishwa kwa Kihausa

12:41 - December 30, 2010
Habari ID: 2055914
Kitabu chenye anwani ya "Mtume Muhammad SAW katika Ukristo" kilichoandikwa na hayati Ahmad Deedat kimetarjumiwa kwa lugha ya Kihausa nchini Nigeria.
Kitabu hicho kilichoandikwa kwa Kiingereza na hayati Ahmad Deedat msomi wa Afrika Kusini kimetarjumiwa kwa Kihausa na mfasiri Muislamu kutoka Nigeria Mohammad Sani Abubakr .
Kitabu hicho kimechapishwa kwa lengo la kuwaelimisha wanaozungumza lugha ya Hausa kuwa kubaathiwa Mtume wa Uislamu (SAW) kumebashiriwa katika kitabu kitakatifu cha Wakristo.
Wahubiri Wakristo wamekuwa wakieneza propaganda potofu za dini yao miongoni mwa Wahausa ambao aghalabu ni Waislamu na hivyo kitabu hicho kinasisitiza kuwa Mtume Muhammad SAW ndio Mtume wa mwisho wa Mwenyezi Mungu.
Mfasiri wa kitabu hicho anaamini kuwa kitaweza kufafanua zaidi ukweli wa Uislamu na kwamba kinatoa majibu kwa maswali mengi kuhusu suala la Utume.
720290
captcha