IQNA

Kitabu cha "Fiqhi ya Kiislamu kwa Mtazamo wa Kimataifa"

13:01 - January 20, 2011
Habari ID: 2067830
Shirika la Kiislamu ya Elimu, Sayansi na Utamaduni ISESCO limechapisha kitabu chenye anwani ya "Fiqhi ya Kiislamu kwa Mtazamo wa Kimataifa".
Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, kitabu hicho kimeandikwa na Christopher Weeramatnry Mkuu wa Zamani wa Mahakama ya Kimataifa ya Uadilifu ICJ ambaye aliwahi kuwa jaji katika Mahakama Kuu ya Sri Lanka. Tafsiri ya Kiarabu ya kitabu hicho iliyopewa jina la Al-Fiqh Al-Islami Min Mandouril Alami imetayarishwa na Dr. Ahmed el Alaoui.
Kitabu kingine ambacho kimechapishwa na ISESCO hivi karibuni ni " Asalat Al-Madrassa Al-Malikia Al Fasia' yaani 'Chimbuko cha Shule ya al Malikia ya Fez' nchini Morocco.
Kitabu hicho kimechapishwa kwa ushirikiano kati ya serikali ya Morocco na ISESCO kwa mnasaba wa mji wa Fez kuwa Mji Mkuu wa Utamaduni wa Kiislamu katika nchi za Kiarabu mwaka 2007.
733570
captcha