IQNA

Maulidi ya Mtume kufanyika Chuo Kikuu cha Kiislamu nchini Pakistan

10:52 - February 09, 2011
Habari ID: 2078223
Akademia ya al Daawa ya Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kiislamu (IIU) nchini Pakistan itakuwa na sherehe za siku tano za kuadhimisha Maulidi ya Mtume Muhammad (saw) katika mwezi wa Rabiul Awwal.
Kituo cha upashaji habari cha The News kimeripoti kuwa sherehe za siku tano za Maulidi ya Mtume zitafanyika katika Msikiti wa Faisal wa chuo hicho kwa shabaha ya kueneza amani na utulivu kwa mujibu wa mafundisho ya Mtume Mtukufu (saw).
Mkurugenzi wa Akademia ya al Daawa Sajid al Rahman amesema kuwa sherehe hizo zitachunguza sehemu mbalimbali za maisha ya Mtume Muhammad (saw) na mafundisho ya Kiislamu ya kuongoza kizazi cha vijana.
Vilevile kutakuwepo maonyesho ya vitabu yatakayoshirikisha makampuni na taasisi za uchapishaji za Pakistan. Sehemu nyingine ya ratiba za sherehe hizo ni kiraa ya Qur’ani Tukufu itakayofanyika katika ukumbi wa IQbal Lahori na kuwashirikisha makarii mashuhuri wa Pakistan. 744495

captcha