Kongamano hilo ni sehemu ya silsila ya vikao vinavyochunguza sira ya Mtume Muhammad (saw) katika vitabu vya Kifaransa, Kiingereza na fasihi ya Kiarabu, maandiko ya Kijerumani na Kihispania na maandiko ya wasomi wa Kimarekani. Vikao hivyo vilianza mwaka 2004 katika Chuo Kikuu cha Muhammad bin Abdullah.
Kongamano hilo litafanyika kuwaenzi waandishi wa Kiholanzi na juhudi zao za kuchunguza maisha ya Nabii Muhammad (saw) na uchunguzi kuhusu masuala ya Mashariki.
Malengo mengine ya kongamano hilo ni kuhamasisha watafiti wa Uholanzi kutalii na kuchunguza sira na maisha ya Mtume Muhammad (saw). 744588