IQNA

Msikiti wa Rasul al-A'dham (saw) kufunguliwa Saihat, Saudi Arabia

16:29 - February 15, 2011
Habari ID: 2081145
Idara inayosimamia Msikiti wa Rasul al-A'dham katika mji wa Kishia wa Saihat nchini Saudi Arabia imesema kuwa ujenzi wa msikiti huo umekamilika na kwamba utafunguliwa tarere 21 Februari ambayo ni siku ya kuadhimishwa Maulidi na kuzaliwa Mtume Mtukufu (saw).
Uandaaji wa sherehe za ufunguzi wa msikiti huo unashughulikiwa na Jumuiya ya Kiutamaduni ya Mtume Mtukufu (saw) ya mji wa Saihat.
Jumuiya hiyo imewataka wanafikra, wanazuoni na wasomi wa Kiislamu kushiriki kwa wingi katika sherehe ya ufunguzi wa msikiti huo na kutoa mchango na fikra zao kuhusu jinsi ya kufanikisha shughuli zake.
Imesema lengo la kutengwa siku ya Miladu Nabii kuwa siku ya kufunguliwa msikiti huo ni kuambatanisha shughuli zake na sira pamoja na miongozo ya Mtume Mtukufu Muhammad (saw). 747771
captcha