IQNA

Msikiti mpya kujengwa Sharjah

16:02 - February 16, 2011
Habari ID: 2081996
Shughuli za ujenzi wa msikiti mpya wa Sharjah katika Umoja wa Falme za Kiarabu zilizinduliwa hapo jana Jumanne na Swagr bin Muhammad al-Qasimi, Katibu Mkuu wa Taasisi ya Wakfu ya Sharjah.
Kwa mujibu wa gazeti la Khaleej Times, msikiti huo ambao utakuwa na uwezo wa kubeba watu 900 utajengwa kwa msingi wa usanifu majengo wa Kiislamu.
Hassan Abdu Rahman Swa'b, mkuu wa Mfuko wa Uwekezaji na Wakfu wa Sharjah amesema kuwa ujenzi wa msikiti huo utakamilika katika kipindi cha mwaka mmoja na nusu ujao.
Ujenzi wake unakadiriwa kugharimu dirhamu milioni 6 za Imarati. 748816
captcha