Tamasha hilo lilianza siku ya Jumatatu Februari na litaendelea hadi siku ya Jumapili Februari 20. Makundi mbalimbali ya uimbaji kasida na usomaji mashairi kama ya Lu'lu' al Batul na Dar al-Wadia' yatashiriki kwenye tamasha hilo kwa lengo la kuwatumbuiza washiriki.
Mbali na kutekeleza vipindi mbalimbali vya burudani na furaha, wanawake watakaoshiriki kwenye tamasha hilo pia watatoa hotuba mbalimbali za kumsifu Mtume (saw) na kubainisha fadhila zake za kimaanawi. 748980