IQNA

Masomo ya Qur'ani kutolewa Texas

14:51 - March 13, 2011
Habari ID: 2094980
Mafunzo ya muda ya Qur'ani Tukufu yatafanyika kuanzia tarehe 3 Juni hadi Julai Mosi katika Taasisi ya Kiislamu ya Texas nchini Marekani.
Kituo cha Bayyinah kimeripoti kuwa mafunzo ya lugha ya Kiarabu na misingi ya tafsiri ya Qur'ani yatatolewa katika masomo hayo yatakayosimamiwa na Jumuiya ya Bayyinah ya Marekani.
Mazsomo hayo yatatolewa kwa lengo la kutoa fursa ya kujifunza lugha ya Kiarabu na sayansi za Qur'ani kwa watu wa eneo hilo. Walimu na wataalamu wa tafsiri na lugha ya Kiarabu watashiriki katika kutoa mafunzo hayo. 762637

captcha