IQNA

Maonyesho ya kaligrafia ya Kiislamu yaanza Pakistan

16:50 - April 04, 2011
Habari ID: 2100526
Maonyesho ya kaligrafia ya Kiislamu yameanza leo Jumatatu huko katika mji mkuu wa Pakistan Islamabad.
Michoro na maandishi mbalimbali ya aya za Qur'ani Tukufu, sunna za Mtume (saw), dua na mashairi kwa lugha za Kiarabu na Kifarsi yanaonyeshwa katika maonyesho hayo. Kaligrafia hiyo ya Kiislamu imepambwa kwa maandishi na kazi za mikono za kuvutia na hasa zile zinazohusiana na utumiwaji wa maji ya dhahabu katika maandishi ya sanaa hiyo ya Kiislamu. Maonyesho hayo yamepangwa kumalizika tarehe 9 Aprili. 768572
captcha