IQNA

Maonyesho ya kwanza ya ufumaji wa Kiislamu kufanyika London

12:12 - April 10, 2011
Habari ID: 2103261
Maonyesho ya kwanza ya ufumaji na bidhaa za kibiashara za Kiislamu yamepangwa kufanyika tarehe 5 Mei katika jumba la maonyesho la Francisca Galloway mjini London.
Kwa mujibu wa tovuti ya Islamic Art Magazine nguo na ufumaji wa kale wa Kiislamu unaohusiana na karne za 14 hadi 19 Milaadia kutoka pembe zote za dunia utaonyeshwa katika maonyesho hayo. Nguo na ufumaji wa falme za Misri, Hipania ya Kiislamu, Wamogholi nchini India, Wasafawi nchini Iran na Waothmani huko Uturuki utaonyeshwa kwa mara ya kwanza katika maonyesho hayo. Maonyeshoa hayo ambayo yameandaliwa kwa ajili ya kuonyesha umuhimu wa nguo na ufumaji katika maisha ya kiuchumi na kijamii ya Waislamu yatamalizika tarehe 6 Mei. 771236
captcha