Kituo cha Sociorel kimeripoti kuwa nakala asili ya insaiklopidia hiyo ilitayarishwa na zaidi ya wahakiki 900 kati ya mwaka 2003 hadi 2007 na inajumuisha makala 1246 katika juzuu 6.
Insaiklopidia hiyo ina makala kuhusu maisha ya wanawake wa Kiislamu katika nchi mbalimbali za Kiislamu na zisizokuwa za Kiislamu ambazo zimeandikwa na wahakiki wa vyuo vikuu kutoka pembe mbalimbali duniani.
Insaiklopidia hiyo pia ina makala kuhusu shughuli wa wanawake wa Kiislamu katika nyanja za siasa, uchumi, jamii, sheria, tiba na sayansi za kisasa. 785094