Ahmad al Tayyib ambaye jana alikuwa akihutubia kikao cha maulamaa, wanafikra na waandishi habari wa Misri mjini Cairo alivitaka vyombo vya habari kutangaza fikra za al Azhar na mitazamo ya wastani.
Vilevile Sheikh wa al Azhar na maulamaa waliohudhuria kikao hicho wamevitaka vyombo vya habari kueneza moyo wa kuvumiliana na mitazamo ya wastani na kujibu fatuwa zisizokuwa sahihi.
Kikao hicho ni katika ajenda ya al Azhar ya kuitisha mazungumzo kati ya wasomi na maulamaa wa Misri kwa ajili ya kufikia mtazamo mmoja kuhusu njia za ustawi na maendeleo ya Misri. 807853