IQNA

18:21 - June 15, 2011
Habari ID: 2138974

Pakistan kuandaa kikao cha mawaziri wa nchi za Kiislamu

Akizungumza hapo jana Jumanne na balozi wa Saudi Arabia nchini Pakistan, Firdous Ashiq Awan, Waziri wa Habari wa nchi hiyo ametangaza hamu ya nchi yake ya kuandaa kikao kijacho cha Mawaziri wa Habari wa Nchi za Kiislamu.

Akibainisha zaidi suala hilo, waziri huyo amesema kuwa zama hizi ni zama za upashaji habari na vyombo vya habari na kwamba nchi za Kiislamu zinapasa kufanya juhudi za kuimarisha vyombo vya habari vya ulimwengu wa Kiislamu kwa kuviwezesha kunufaika na teknolojia ya kisasa kabisa katika uwanja huo. Firdous Ashiq amesema katika mazungumzo hayo kwamba nchi yake ina hamu kubwa ya kubadilishana wataalamu wa masuala ya habari na nchi nyinginezo za Kiislamu.
Tunakumbusha hapa kwamba duru ya nane ya Mawaziri wa Habari wa Nchi za Kiislamu ilifanyika yapata miaka mitatu iliyopita huko Rabat, mji mkuu wa Morocco. 809214
captcha