IQNA

Mashindano ya kitaifa ya Qur'ani na Hadithi kufanyika Comoro

18:18 - July 06, 2011
Habari ID: 2150251
Mashindano ya kitaifa ya hifdhi ya Qur'ani na Hadithi yatafanyika tarehe 17 Julai katika visiwa vya Comoro kwa ushirikiano wa Jumuiya ya Masuala ya Kheri ya Sheikh Thani bin Abdullah (RAF) ya Qatar.
Gazeti la al Sharq la Qatar limeripoti kuwa mashindano hayo ya hifdhi ya Qur'ani na Hadithi ya Comoro yatasimamiwa na Wizara ya Mambo ya Masuala ya Kiislamu na Jumuiya ya Masuala ya Kheri ya Comoro.
Mwakilishi wa jumuiya ya RAF Muhammad Salah Ibrahim amesema kuwa mashindano hayo yatajumuisha hifdhi ya Qur'ani na Hadithi na maarifa ya maswahaba wa Mtume Muhammad (saw). Ameongeza kuwa mashindano hayo yatawashirikisha wanawake na wanaume.
Mwakilishi wa RAF amesema kuwa awamu ya awali ya mashindano hayo itafanyika mwezi Ramadhani mwaka huu katika makao ya Wizara ya Masuala ya Kiislamu ya Comoro.
Muhammad Saleh Ibrahim amesema sherehe za kufunga mahindano hayo zitahudhuriwa na Rais Ikililou Dhoinine wa Comoro. 820400


captcha