IQNA

Makala 75 katika kongamano la Imam Mahdi AS Tehran

9:15 - July 14, 2011
Habari ID: 2154234
Mkutano wa Saba wa Kimataifa ya Imam Mahdi AS unafanyika Tehran huku kukiwa na makala 75 za watafiti kutoka Iran na nchi kadhaa duniani.
Kati ya mada zitakazojadiliwa katika kongamano hilo ni 'Vyombo vya Habari na Imam Mahdi AS', 'Nafasi ya Vyombo vya Habari Katika Kuandaa Mazingira ya Kudhihiri Imam Mahdi' na 'Mikakati ya Vyombo vya Habari katika Kuandaa Mazingira ya Kurejea Imam Mahdi'.
Mada zingine katika kongamano hilo zitakuwa ni pamoja na 'Nafasi ya Vyombo vya Habari katika kustawisha utamaduni wa Imam Mahdi', 'Uwezo na Vizingiti vya Vyombo vya Habari katika kaundaa mazingira ya kurejea Imam Mahdi'.
Kongamano hilo litafanyika Alhamisi na Ijumaa Julai 14-15 mjini Tehran.
825217






captcha