Abuzar Khayyati amesema kuwa ukumbi wenye mita 2500 mraba umetengwa kwa ajili ya teknolojia ya dijitali katika maonyesho hayo ambapo taasisi 100 za Qur'ani zitashiriki.
"Sehemu iliyotengwa haitoshi kwa ajili ya taasisi za Qur'ani zinazoshiriki na hivyo kunapaswa kuchukuliwa hatua za kuwezesha taasisi nyingi zaidi kushiriki katika maonyesho haya ya kimataifa", ameongeza.
Maonyesho ya 19 ya Kimataifa ya Qur'ani yataanza mwishoni mwa mwezi wa Shaaban hadi tarehe 15 ya mwezi ntukufu wa Ramadhani katika Ukumbi wa Sala wa Imam Khomeini mjini Tehran.
824677