IQNA

Shule za sekondari Iran kuanza kwa mafunzo ya Qur’ani

13:10 - July 19, 2011
Habari ID: 2156382
Kuanzia mwaka ujao wa masomo, shule zote za sekondari za Iran zitaanza klasi kwa somo la Qur’ani la dakika tano.
Haya ni kwa mujibu wa afisa wa Wizara ya Elimu ya Iran Bi. Mardhiya Mesgarzadeh ambaye ameongeza kuwa lengo la somo hilo fupi ni kutoa mafunzo ya misingi ya Qur’ani kwa wanafunzi.
“Somo hilo litajumuisha pia kiraa ya Qur’ani Tukufu”, ameongeza.
Kwa mujibu wa mpango huo waalimu wa masomo yote yakiwemo hisabati, sana, Lugha ya Kifarsi n.k wataanza somo kwa kusoma aya chache za Qur’ani na kuelezea maana yake.
Amesema tayari warsha zimefanyika katika shule za upili ili kujadili njia za utekelezaji mpango huo.
827066
captcha