IQNA

Kongamano la 9 la Qur'ani kufanyika Saihat

18:55 - August 06, 2011
Habari ID: 2166042
Jumuiya ya Qur'ani Tukufu ya Waislamu wa madhehebu ya Shia wa mashariki wa Saudi Arabia imetangaza kuwa inajitayarisha kwa ajili ya kusimamia kongamano la 9 la kila mwaka la Qur'ani Tukufu.
Kongamano hilo linasimamiwa na Jumuiya ya Qur'ani ya Saihat ikishirikiana na maulamaa na watafiti wa masuala ya Qur'ani katika Msikiti wa Rasurul Aadham SAW katika mji wa Saihat.
Kongamano hilo linalofanyika kila mwaka katika nusu ya mwezi mtukufu wa Ramadhani huhudhuriwa na shakhsia mashuhuri wa mikoa ya mashariki mwa Saudia yenye Waislamu wengi wa madhehebu ya Shia. Mada kuu ya kongamano la mwaka huu ni amani ya kijamii na ushirikiano na kuishi kwa amani jamii zenye tamaduni tofauti katika mtazamo wa Qur'ani Tukufu. 838035
captcha