Habari zinasema kuwa mkusanyiko huo ulifanyika ndani ya Msikiti wa al Azhar kuonyesha upinzani dhidi ya uhalifu na jinai za Israel na ulitoa wito wa kufukuzwa balozi wa utawala huo ghasibu nchini Misri.
Waandamanaji hao waliitaka serikali ya Cairo isimamishe uuzaji wa gesi ya Misri kwa utawala ghasibu wa Israel na kulaani jinai za utawala huo katika mpaka wa Misri na Ukanda wa Gaza.
Mwenyekiti wa chama cha Amal Majdi Hussein mesisitiza mbele ya mjumuiko huo kwamba eneo la Sinai linapaswa kuondolewa katika udibiti wa Israel. Ameongeza kuwa baada ya ushindi wa mapinduzi ya wananchi, Misri inapaswa kuchukua hatua kali zaidi za kukabiliana na uhalifu na uchokozi wa Israel.
Kiongozi wa chama cha Amal amesisitiza kuwa kunyamaza kimya kwa serikali ya Misri mbele ya jinai na mauaji yaliyofanywa na utawala ghasibu wa Israel katika mpaka wa nchi hiyo na Ukanda wa Gaza ni jambo ambalo haliwezi kukubaliwa. 850492