IQNA

Haram ya Imam Ridha (AS) imeandaa Hafla ya Qur’ani ya Arbaeen

23:03 - July 01, 2026
Habari ID: 3482427
IQNA – Hafla maalumu ya Qur’ani inayolenga kuenzi hadhi ya juu ya mashahidi, kuendeleza utamaduni wa Qur’ani Tukufu na Ahlul Bayt (AS), pamoja na kuzindua rasmi programu za Qur’ani za Arbaeen, imefanyika Jumatano katika Haram Takatifu ya Imam Ridha (AS) kwa ushiriki wa maqari, mahafidhi, wanaharakati wa Qur’ani na wapenda dini.

Hafla hiyo imefanyika sambamba na kumbukumbu ya shahada ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, mashahidi wa Vita vya Tatu vya Kulazimishwa, pamoja na kuanza kwa programu za Qur’ani za Arbaeeni. Mkusanyiko huo wa Qur’ani unaobeba anuani “Pamoja na Qur’ani katika Njia ya Peponi” umeandaliwa na Kamati ya Shughuli za Qur’ani ya Makao Makuu ya Utamaduni wa Arbaeen.

Sherehe hiyo, itakayohudhuriwa na kundi la maqari, mahafidhi na wanazuoni wa Qur’ani kutoka ndani na nje ya nchi, imefanyika kuanzia saa 11:00 jioni hadi saa 12:30 jioni kwa saa za eneo hilo katika ukumbi wa Imam Khomeini (RA) ndani ya Haram Takatifu.

Katika mkusanyiko huo wa Qur’ani, qari mashuhuri Javad Panahi pamoja na hafidhi wa Qur’ani Reza Golshahi wamesoma aya za Qur’ani Tukufu. Aidha, kundi la kwaya la “Nasim Rezvan” limetoa onesho maalumu kama sehemu ya ratiba ya hafla hiyo.

Katika kipengele kingine cha hafla hiyo, Hujjatul-Islam Mahmoud Mohammadian ambaye pia ni hafidhi wa Qur’ani, sambamba na maqari mashuhuri Reza Shahmiveh na Javad Soleimani, wamesoma aya  za Qur’ani Tukufu.

Hafla hiyo imerushwa mubashara kupitia kituo cha televisheni cha Qur’an na Ma’arif pamoja na Radio Qur’an.

3498036

Habari zinazohusiana
captcha