IQNA

Iran kuongeza idadi ya waliohifadhi Qur'ani

14:50 - August 29, 2011
Habari ID: 2178789
Mwakilishi wa Waliul Faqih katika Shirika la Waqfu la Iran amesema kuwa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu anatazamia kuwa suala la kuongeza idadi ya Wairani waliohifadhi Qur'ani litapewe umuhimu.
Hujjatul Islam wal Muslimin Ali Muhammadi akizungumza na IQNA amesema kuwa, wakati Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Ali Khamenei alipokutana na Jamii ya Wanaharakati wa Qur'ani nchini hivi karibuni alisisitiza kuhusu suala la kuongezwa idadi ya waliohifadhi Qur'ani nchini Iran.
Amesema Shirika la Waqfu sasa linatoa kipaumbele kwa suala la kutekeleza nasaha za Kiongozi Muadhamu. Amesema, sasa hivi kuna mikakati ya kuongeza idadi ya waliohifadhi Qur'ani nchini.
851491
captcha