IQNA

Waislamu wa kweli hufuata Qur’ani kwa vitendo na si maneno

15:31 - September 07, 2011
Habari ID: 2182836
Kupuuza mafundisho ya Qur’ani Tukufu kunatokana na kutofuata misingi yake katika maisha halisi. Hakuna haja ya maneno tu bila vitendo .
Haya ni kwa mujibu wa Ali Pashaee, Mkuu wa Taasisi ya Familia na Qur’ani ya Iran. Pashaee ametoa wito kwa maafisa wa Wizara ya Utamaduni na Mwongozo wa Kiislamu kushirikiana na taasi za Kiislamu nchini kama vile Shirika la Ustawi wa Kiislamu ili kuhakikisha kuwa mafundisho ya Qur’ani yanaonekana kivitendo katika maisha ya kila siku ya wananchi.
Amesema pamoja na kuwepo vituo 3000 vikubwa vya Qur’ani nchini Iran bado juhudu zaidi zinahitajika ili kuimarisha mafundisho ya Qur’ani na kuhakikisha kuwa miongozo wa kitabu hicho kitukufu inatekelezwa katika maisha ya kila siku.
‘Leo maadui wanajaribu kupotosha Qur’ani Tukufu kwa mtazamo wa utekelezaji na hivyo kuna haja kwa wataalamu wa Qur’ani kuongeza juhudi katika uwanja huo. 853406
captcha