IQNA

Vikao vya kiraa ya Qur'ani vyafanyika katika misikiti ya Marekani

15:46 - September 26, 2011
Habari ID: 2193704
Vikao vya kiraa ya Qur'ani Tukufu vinafanyika katika misikiti ya miji mbalimbali ya Marekani.
Kituo cha habari cha Sunniforum kimeripoti kuwa vikao hivyo vya Qur'ani vilivyoanza tarehe 19 Septemba vitaendelea hadi tarehe 9 Oktoba.
Vikao hivyo vinafanyika katika misikiti ya New York, New Jersey na Pennsylvania na vinasimamiwa na Kituo cha Kiislamu cha Asifa chenye makao yake mjini New York.
Mkuu wa Madrasa ya Rahmaniya ya Dhaka, Bangladesh Hafidh Zubair Ansari na khatibu wa Msikiti wa Baitul Maamur wanatoa darasa za tafsiri ya Qur'ani katika vikao hivyo. 867421

captcha