Serikali ya Sudan imetangaza kuwa safari hiyo ambayo pia itawajumuisha viongozi wengine wa ngazi za juu wa serikali ya Khartoum itaendelea kwa muda wa siku mbili.
Mazungumzo hayo ya siku mbili yanafanyika huku Qatar ikiwa mpatanishi kati ya serikali ya Khartoum na waasi wa eneo la Darfur la magharibi mwa nchi hiyo.
Miezi kadhaa iliyopita Qatar ilikuwa mwenyeji wa pande hizo hasimu za Sudan ambapo serikali ya Khartoum hatimaye ilifikia mapatano ya suluhu na Harakati ya Uhuru na Uadilifu ya Darfur. 876885