IQNA

Shalit:

Hamas wameamilia nami kwa wema

22:00 - October 18, 2011
Habari ID: 2207551
Askari wa utawala wa Kizayuni wa Israel aliyekuwa anashikiliwa mateka na Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas kwa kipindi cha miaka mitano amesema kuwa wanachama wa harakati hiyo waliamiliana naye kwa wema na vizuri katika kipindi chote alichokuwa mateka.
Gelad Shalit ambaye ameachiwa huru leo katika utekelezaji wa makubaliano ya kubadilishana mateka kati ya utawala haramu wa Israel na harakati ya Hamas, amepongeza harakati hiyo kwa mwenendo mzuri wa wanachama wake.
Amesema kua katika kipindi chote cha miaka mitano ya kuwa mateka, hamas imeamiliana nami vizuri.
Shalit pia amewalaumu viongozi wa Israel na kusema kuwa miaka 5 iliyopita Israel ingeweza kumkomboa yeye kwa kuwaachia huru mateka wa Kipalestina lakini viongozi wa Tel Aviv wamechukua hatua kwa kuchelewa. 882592


captcha