IQNA

Maonyesho ya nakala ya kale ya Qur'ani katika intaneti

16:26 - October 26, 2011
Habari ID: 2212452
Nakala ya kale na nadra ya Qur'ani yenye umri wa miaka 500 inaonyeshwa katika mtandao wa intaneti kwa hima ya Chuo Kikuu cha Manchester huko Uingereza.
Msemaji wa chuo hicho amesema kuwa nakala hiyo iliyoandikwa kwa hati za mkono ni miongoni mwa nuskha nadra na muhimu mno za Qur'ani duniani.
Ameongeza kuwa nalaka hiyo pamoja na nakshi zake iliandikwa kwa hati za mkono miaka 500 iliyopita na haijawahi kuonyeshwa hata mara moja kutokana na ulaini na muundo wa karatasi zake.
Msemaji wa Chuo Kikuu cha Manchester amesema kuwa nakala hiyo nadra ya Qur'ani Tukufu ina kurasa 470 na inahifadhiwa katika maktaba ya chuo hicho.
Licha ya hitilafu zilizopo kati ya wanahistoria kuhusu historia ya kuandikwa Qur'ani hiyo, taarifa zilizopatikana zinaonyesha kuwa nakala hiyo iliandikwa katika karne ya 14 au 15 Miladia. 887855

captcha