IQNA

Nakala milioni 20 za Qur'ani zatolewa kwa mahujaji

19:12 - November 12, 2011
Habari ID: 2221246
Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kiislamu ya Saudi Arabia imegawa nakala milioni 20 za kitabu cha Qur'ani Tukufu na vitabu vya kidini kwa mahujaji waliokwenda kujihi mwaka huu.
Mshauri wa Waziri wa Wakfu wa Saudia Talal bin Ahmad Akiil amesema nakala hizo za Qur'ani na vitabu vya kidini zimetolewa kwa mahujaji katika viwanja vya ndege wakati wanapokuwa wakirejea nchini kwao.
Amesema katika kipindi chote cha ibada ya hija nakala laki mbili na nusu za Qur'ani Tukufu, tarjumi yake kwa lugha mbalimbali na vitabu vya kidini zilikuwa zikitolewa kila siku kwa mahujaji wa Nyumba ya Mwenyezi Mungu. 897197

captcha