IQNA

Mashindano ya Qur’ani ya Ras Al Khaimah Imarati

17:58 - November 14, 2011
Habari ID: 2222724
Mashindano ya 12 ya Kimataifa ya Qur’ani ya Ras al Khaimah yataanza Novemba 15 kukiwa na vitengo viwili vilivyoongezwa.
Kwa mujibu wa gazeti la Al Ettehad mashindano hayo yanafanyika chini ya usimamizi wa Sheikh Sa’ud bin Saqar Al-Qasimi, mtawala wa Ras Al-Khaimah.
Umar bin Abdul Aziz Al-Ghasemi, Katibu Mkuu wa mashindano hayo ambaye pia ni mkuu wa Taasisi ya Qur’ani ya Ras Al Khaimah amesema mashindano hayo yatajumuisha vitengo vya kuhifadhi Qur’ani kamili, juzuu 20,10, 5 na 3. Aidha kutakuwa na mashindano ya tajweed na tarteel.
Mashindano hayo yanatazamiwa kumalizika Novemba 24.
897624
captcha