IQNA

Tamasha ya Kitaifa ya Qur’ani ya wanafunzi yamalizika Iran

16:37 - November 26, 2011
Habari ID: 2228500
Tamasha ya Kitaifa ya Qur’ani ya Wanafunzi nchini Iran imemalizika katika sherehe zilizofanyika Ijumaa katika mji mtakatifu wa Mash'had.
Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, sherehe hiyo ilianza kwa kisomo cha Qur’ani Tukufu na kufuatiwa na ripoti iliyotolewa na Saniepur, katibu wa tamasha hiyo.
Wengine waliozungumza katika hafla hiyo ni Naibu Waziri wa Elimu, Naibu Waziri wa Utamaduni na Mkuu wa Kituo cha Kuratibu, Kustawisha na Kueneza Harakati za Qur’ani nchini Iran.
Tamasha hiyo ilifanyika katika Chuo Kikuu cha Ferdowsi mjini Mash'had kuanzia tarehe 23 Novemba na ilijumuisha pia mashindano ya Qur’ani Tukufu.
904719
captcha