IQNA

18:59 - February 18, 2012
Habari ID: 2276391
Hania:

Taifa la Palestina litawakomboa mateka wanaoshikiliwa katika jela za Israel

Waziri Mkuu wa serikali halali ya Palestina Ismail Hania amesema tangazo la mshikamano wa Wapalestina na Adnan Khidhr, mateka wa Kipalestina mbaye ameanza mgomo wa chakula tangu siku 62 zilizopita, ni ujumbe muhimu kwamba taifa la Palestina linashikamana na suala la kukomboa mateka wanaoshikiliwa katika korokoro za Israel.

Ismail Hania amesema kuwa matabaka yote ya wananchi na makundi mbalimbali ya mapambano ya ukombozi yangali yanashikamana na ahadi ya kuwakomboa mateka wa Kipalestina wanaoshikiliwa katika korokoro za Israel.
Amesisitiza kuwa wananchi wa Palestina wataendelea kuwatetea mateka hao hadi pale watakapoachiwa huru.
Hania amesema irada ya mateka wa Kipalestina walioko katika jela za utawala ghasibu wa Israel itashinda na Wapalestina wote wako katika handaki moja katika kupinga ukatili na unyama wa Israel dhidi ya mateka wa Kipalestina. 955361



captcha