IQNA

10:55 - March 18, 2012
Habari ID: 2293296

Wananchi wa Tunisia waandamana wakitaka sheria za Kiislamu

Maelfu ya wananchi wa Tunisia wameandamana nje ya jengo la bunge mjini Tunis wakitaka sheria za Kiislamu zitekelezwe nchini humo.

Katika maandamano hayo wananchi wametangaza bayana kwamba watapinga katiba yoyote itakayopitishwa pasina kuwepo sheria za Kiislamu ndani yake. Waandamanaji wametoa nara kama vile, 'Wananchi wanataka sheria za Mwenyezi Mungu zitekelezwe' na 'Tunisia ni nchi ya Kiislamu'. Aidha makundi zaidi 200 ya kisiasa na kiraia yametia saini taarifa ya kutaka sheria za Kiislamu zitekelezwe nchini humo.
Bunge la Waasisi la Tunisia liko katika mkakati wa kuandika katiba mpya ya nchi hiyo. Zoezi la kuandika katiba hiyo linatazamiwa kumalizika katikati ya mwaka huu wa 2012.
Utawala wa kiimla wa Tunisia ulipinduliwa Januari 14 mwaka 2011 kufuatia mwamko wa Kiislamu wa wananchi. Dikteta wa Tunisia aliyetimuliwa madarakani Zine el Abidine Ben Ali amepewa hifadhi na utawala wa Saudi Arabia.
973109
captcha