IQNA

16:52 - April 07, 2012
Habari ID: 2299239

'Uingiliaji wa kigeni nchini Syria utaharibu hali ya mambo'

Khatibu wa muda wa Sala ya Ijumaa hapa mjini Tehran amesema leo kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaunga mkono mageuzi ya ndani nchini Syria lakini ametahadharisha kuwa uingiliaji wowote wa kigeni utazidi kuharibu hali ya mambo.

Ayatullah Ahmad Khatami ameongeza kuwa Syria inaandamwa na madola ya Magharibi pamoja na baadhi ya nchi za Kiarabu kutokana na misimamo yake ya kuunga mkono mapambano dhidi ya utawala haramu wa Israel. Ayatullah Khatami amezionya nchi za Kiarabu zikiongozwa na Saudi Arabia akisema kuwa moto wanaojaribu kuuwasha huko Syria utakuwa kama mtego wa panya ambao hunasa waliokuwemo na wasiokuwemo.
Khatibu wa muda wa Sala ya Ijumaa ya Tehran aidha amekumbusha kuwa baadhi ya nchi za Kiarabu zinaisakama Syria ili kupoza moto unaowaka katika nchi zao lakini amesisitiza kuwa mwamko wa Kiislamu utawafagia madikteta wote katika eneo la Mashariki ya Kati na ulimwengu wa kiarabu kwa ujumla.
Vilevile amekosoa hatua ya nchi za Kiarabu ya kupuuza mauaji na ukandamizaji unaofanywa na utawala wa kifalme wa Bahrain dhidi ya raia wa nchi hiyo na kulaani uvamizi wa Saudi Arabia ambayo imetuma majeshi huko Bahrain kukandamiza wananchi wa nchi hiyo.
979335
captcha