IQNA

18:08 - May 05, 2012
Habari ID: 2318040
Hatibu wa Swala ya Ijumaa ya Tehran:

Waislamu duniani wakabiliane na wanaoivunjia heshima Qur'ani

Khatibu wa Sala ya Ijumaa Tehran Ayatullah Sayyid Ahmad Khatami amelaani vikali kitendo cha kasisi wa Marekani cha kuchoma moto nakala za Qur'ani Tukufu na ametoa wito kwa Waislamu wote duniani kukabiliana na kitendo hicho kichafu.

Khatibu wa Sala ya Ijumaa ya Tehran amesema serikali ya Marekani ni mshirika katika kuvunjiwa heshima Qur'ani na amehoji ni kwa nini Wamarekani ambao hawawezi hata kustahamili mjadala kuhusu maudhui ya 'Holocaust' wanavunjia heshima Kitabu Kitakatifu cha Waislamu zaidi ya bilioni moja na nusu duniani?
Ayatullah Khatami pia amekosoa kimya cha Wakristo duniani kufuatia hatua ya kasisi Mkristo Marekani kuivunjia heshima Qur'ani Tukufu.
Kuhusu uchaguzi ujao wa rais nchini Misri, Ayatullah Khatami amesema taifa lililostaarabika la Misri halitaruhusu mapinduzi ya wananchi yatekwe. Ameongeza kuwa waliohudumu katika utawala wa dikteta Mubarak hawapasi kuchaguliwa na kuongeza kuwa Wamisri watamchagua rais anayepinga ubeberu na Uzayuni.
Kuhusu kadhia ya Bahrain, Ayatullah Khatami amesema kuwa, taifa la Iran litaunga mkono taifa linalodhulimiwa la Bahrain kama linavyounga mkono taifa linalodhulumiwa la Palestina.

999654
captcha