IQNA

Mafunzo ya Qur'ani Tukufu maalumu kwa miezi ya Shaaban na Ramadhani nchini Pakistan

17:26 - June 20, 2012
Habari ID: 2350824
Taasisi ya Minhaj al-Qur'an ya Pakistan imepanga kuendesha mafunzo ya Qur'ani Tukufu katika maeneo 500 ya nchi hiyo maalumu kwa ajili ya mieizi mitukufu ya Shaaban na Ramadhani.
Akibainisha suala hilo, Twahir Qadiri, mkuu wa taasisi hiyo amesema mafunzo hayo yatatolewa kwa lengo la kueneza mafundisho ya Qur'ani katika maeneo tofauti ya nchi hiyo. Amesema mafunzo hayo yatatolewa katika maeneo ya vijijini hadi miji mikubwa kwa lengo la kuwafundisha wakazi wa maeneo hayo mafundisho muhimu ya kitabu hicho cha mbinguni.
Allama Afdhal Qadir kiongozi mwingine wa taasisi ya Minhajul Qur'an amesema mafunzo hayo yatatolewa kwa madhumuni ya kuwashajiisha watu kujifunza Qur'ani Tukufu (saw). 1034079
captcha