Sheikh Mazin as-Saidi, Mkuu wa Jumuiya ya Qur'ani inayofungamana na Taasisi ya Shahid Sadr wa Pili na anayesimamia mashindano hayo amesema mashindano hayo ya kimataifa yatazishirikisha nchi 26 za Kiarabu na Kiislamu.
Amesema kuongezeka kwa idadi ya nchi zinazoshiriki katika mashindano hayo kunabainisha wazi kuboreka kwa kiwango chake.
Sheikh Mazin as-Saidi amesema duru ya kwanza ya mashindano hayo iliyofanyika katika mwezi mtukufu wa Shaaban mwaka uliopita ilizishirikisha nchi 16. 1038371