IQNA

Maonyesho ya mwandishi Qur'ani wa Iran nchini Qatar

12:44 - July 17, 2012
Habari ID: 2370797
Balozi na mwambata wa kiutamaduni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Falme za Kiarabu siku ya Alkhamisi ijayo wanatazamiwa kushiriki kwenye maonyesho ya sanaa mjini Doha Qatar ambapo msanii mashuhuri wa Iran anatazamiwa kuonyesha kazi zake za uandishi wa Qur'ani kwa kutumia mkono.
Shahrokh Faryusufi msanii mashuhuri wa Iran anatazamiwa kuonyesha kazi zake katika maonyesho hayo ambayo yameandaliwa kwa ushirikiano wa Wizara ya Utamaduni na Sanaa ya Qatar.
Kazi muhimu 30 za waandishi wa Qur'ani zinatazamiwa kuonyeshwa katika maonyesho hayo ya maandishi ya mkono ya aya za Qur'ani Tukufu ambayo yamepangwa kuendelea kwa muda wa wiki moja.
Maonyesho hayo yamepangwa kuanza sambamba na kukaribia mwezi mtukufu wa Ramadhani. 1055056
captcha