Ujumbe wa makari na mahafidh wa Qur'ani kutoka Misri ambao umealikwa humu nchini na Idara ya Masuala ya Qur'ani ya taasisi hiyo utakuwa humu nchini kwa kipindi cha wiki moja.
Swabir Id, Muhammad al-Husseini na Sayyid Ibrahim Warda, makari mashuhuri wa Misri walipata fursa ya kuwafariji hadhirina kwa visimo vyao vya kuvutia vya Qur'ani Tukufu.
Hatimaye hadhirina waliswali swala za adhuhuri na alasiri kwa uimamu wa Ayatullah Taskhiri. 1060609