Sheikh
Taha Noomani, mwanachama wa Jumuiya ya
Wasomaji na Waliohifadhi Qur'ani Misri amesema Sheikh Mustafa Ghalwash atazikwa leo baada ya sala ya Alasiri katika kijiji
alikozaliwa cha Borma katika mkoa wa Gharbiya nchini Misri. Ameongeza kuwa Ijumaa kutafanyika khitam ya marhuma Sheikh Mustafa Ghalwash katika
kijiji hicho.
Ghalwash aliwahi kualikwa kusoma Qur'ani katika nchi mbali mbali kama vile Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Uingereza, Ufaransa na Marekani.
Kuhusu kumbukumbu yake ya safari nchini Iran Ghalwash alisema: "Sijawahi kuona watu wenye kusikilizaj qiraa ya Qur'ani kwa hisia ya dhati ya moyo kama nilivyoona Iran. Naona mustakabali mzuri kwa maquraa nchini Iran kwani wana lahni na tajwidi nzuri sana."