IQNA

Mjue Imam Hussein AS

Sheikhe Mkuu wa Al-Azhar atembelea Msikiti wa Imam Hussein (AS) mjini Cairo

16:28 - May 31, 2022
Habari ID: 3475319
TEHRAN (IQNA)- Mkuu wa Kituo cha Kiislamu cha Al Azhar nchini Misri Sheikh Ahmad Al-Tayyib ameutembelea Msikiti wa Imam Hussein (AS) mjini Cairo na kukagua kazi ya ukarabati iliyofanywa katika msikiti huo na majengo mengine yanayohusiana nao.

جانب من جولة الإمام الأكبر بمسجد الحسين

Kwa mujibu wa taarifa, Sheikh Al-Azhar amejionea dharih (sehemu ya kuzikwa) mpya ya Msikiti wa Imam Hussein (AS) na maeneo mengine ya ndani na nje ya msikiti huo pamoja na ustawi jumla wa Haram hiyo takatifu.

Rais Abdel Fattah al-Sisi hivi karibuni alizindua Msikiti wa Imam Hussein (AS) mjini Cairo muda mfupi baada ya ukarabati wake kukamilika.

Katika uzinduzi huo, rais wa Misri hivi karibuni alitangaza juhudi za serikali ya Misri za kujenga upya maziara na maeneo yote yanayohusiana na Ahlul Bayt (AS) mjini Cairo na maeneo mengine ya Misri.

Katika miaka ya hivi karibuni, serikali ya Misri imeanza mpango mkubwa wa ukarabati wa maeneo matakatifu na misikiti yenye mafungamano na Ahul Baty au watu wa Nyumba ya Mtume Muhammad SAW.

Msikiti wa Imam Hussein (AS) ndio mkubwa zaidi kati ya misikiti ya Ahul Bayt AS, na ulijengwa karne ya sita Hijria.

Kwa mujibu wa baadhi ya riwaya, msikiti huu ni kaburi la kichwa cha Imam Hussein (AS). Msikiti wa Imam Hussein (AS) ni miongoni mwa misikiti muhimu sana katika ulimwengu wa Kiislamu na nchini Misri, na ni kitovu cha qiraa ya Qur'ani Tukufu nchini humo.

الإمام الأكبر يتفقد أعمال التجديد الشاملة بمسجد الحسين صباح اليوم |صور

جانب من جولة الإمام الأكبر بمسجد الحسين

جانب من جولة الإمام الأكبر بمسجد الحسين

4060578

captcha