IQNA

Shule ya Qur’ani yafunguliwa Gaza kwa msaada wa wananchi wa Iran

17:41 - December 17, 2025
Habari ID: 3481675
IQNA – Shule mpya ya Qur’ani imefunguliwa mjini Gaza kwa mchango wa kampeni ya wananchi wa Iran inayojulikana kama “Iran Hamdel” kwa ushirikiano na Taasisi ya Ahl al‑Quran ya Gaza.

Shule hiyo, inayojulikana kama Shule ya Qur'ani ya Sayed Hashem, imeanzishwa kwa lengo la kupanua huduma za kidini na kielimu kwa Watoto Wapalestina na vijana wa Ukanda wa Gaza.

Pia inatoa masomo ya Qur’ani na elimu kwa wanafunzi wa maeneo hayo. Ufunguzi wa kituo hiki cha elimu umepokelewa kwa shukrani kubwa na familia zilizoathiriwa na vita pamoja na wananchi waaminifu wa Gaza City. Uanzishwaji wa shule hii ni sehemu ya shughuli za kitamaduni na kibinadamu za kampeni ya Iran Hamdel, zenye lengo la kuimarisha moyo wa matumaini na uthabiti miongoni mwa watu wa Gaza.

Kampeni hiyo, ambayo imewahi kutekeleza miradi kama hii katika nchi nyingine, inaendelea na dhamira yake ya kuonesha mshikamano wa Wairani na Palestina na kuwaunga mkono Wapalestina kupitia programu mbalimbali za kijamii na kibinadamu. 

3495761

Habari zinazohusiana
Kishikizo: qurani tukufu gaza iran
captcha