
Shule hiyo, inayojulikana kama Shule ya Qur'ani ya Sayed Hashem, imeanzishwa kwa lengo la kupanua huduma za kidini na kielimu kwa Watoto Wapalestina na vijana wa Ukanda wa Gaza.
Pia inatoa masomo ya Qur’ani na elimu kwa wanafunzi wa maeneo hayo. Ufunguzi wa kituo hiki cha elimu umepokelewa kwa shukrani kubwa na familia zilizoathiriwa na vita pamoja na wananchi waaminifu wa Gaza City. Uanzishwaji wa shule hii ni sehemu ya shughuli za kitamaduni na kibinadamu za kampeni ya Iran Hamdel, zenye lengo la kuimarisha moyo wa matumaini na uthabiti miongoni mwa watu wa Gaza.
Kampeni hiyo, ambayo imewahi kutekeleza miradi kama hii katika nchi nyingine, inaendelea na dhamira yake ya kuonesha mshikamano wa Wairani na Palestina na kuwaunga mkono Wapalestina kupitia programu mbalimbali za kijamii na kibinadamu.
3495761